Friday, July 30, 2010

SHILINGI YAUA- SIMBA WA NYIKA



Tuselebuke kizamani-zamani

Kwa ijumaa hii si vibaya tukawasikiliza Simba wa Nyika katika Shilingi Yaua. Gonga hii link hapa chini.

http://www.ntwiga.net/linked_to_audio/Simba_Wanyika-Shilingi_maua_tena_maua

Kuna mtu anaweza nitajia majina yote ama baashi ya kundi la Simba wa Nyika

Labels:

Monday, July 26, 2010

HILI NALO LAWEZA KUWA NENO


DANGER OF USING LAPTOPS ON BED
You may have heard that a good friend of ours in Mequon lost their 25
year old son (Arun Gopal Ratnam) in a fire at home June 4th. This is
what happened. He graduated with MBA from University of
Wisconsin-Madison two weeks earlier and came home. Had a lunch with
his dad at home and decided to go back to to clean up his room at
school. Father told him to wait and see his mother before he goes back
for a few days. He decided to take a snooze while waiting for his mom
to come home from work.

Neighbors called 911 when they saw black smoke coming out of the
house. Their 25 year old son Arun died in the three year old house. It
took several days of investigation to find out the cause of the fire.
It was determined that the fire was caused by lap top in the bed. When
the lap top is on the bed cooling fan does not get air to cool the
computer and that is what caused the fire. He did not even wake up to
get out of the bed he died of carbon monoxide.

The reason I writing this to all of you is that I have seen all of us
using our lap top in bed. Let us all decide and make it a practice not
to do that. Risk is real. Let us make it a rule not to use lap top in
bed or put computer on bed with blankets and pillows around.

Chanzo. E-mail to me.

Labels:

Thursday, July 22, 2010

BRING HIM (MANDELA) BACK HOME

Mwaka 1988 wakati familia yetu ikishi Morogoro wazungu fulani wakimbatana na wakimbizi wa Afrika ya Kusini waliokuwa wakiishi Mazimbu walimpa baba yangu kanda ikiwa na wimbo 'Bring Him Back'. Wimbo ulikuwa na maudhui ya kutaka Nelson Mandela aachiliwe kutoka kifungoni. Hapa chini ni Vidio Yake. Umeimbwa na aliyewahi kuwa mume wa marehemu Miriam Makeba, Hugh Masekela.



Hivi majuzi babu Mandela ametimiza umri ya miaka 92. Nampongeza kwa kumpigia video yii. Kibwagizo kinaenda hivi:

Bring back Nelson Mandela, Bring him back home to Soweto
I want to see him walking down the streets of South Afrika

Bring back Nelson Mandela, Bring him back home to Soweto
I want to see him walking hand in hand with Winnie Mandela




Nelson Mandela na Walter Sisulu wakiwa gerezani

Sauti ya Vuvuzela (Baragumu) inamtakia miaka mingi mbeleni.

Labels: , ,

Tuesday, July 20, 2010

MAPENZI HOSPITALI YA VICHAA

Watu huonyesha upendo kwa njia mbalimbali. Sio lazima wakuonyeshe upendo kwa namna uzitakazo wewe. Sikiliza hii.

Omari na Edna walikuwa wamelazwa hospitali ya vichaa. Siku moja walipokuwa wakipita kando ya bwawa la kuogelea la hospitalini hapo, Omari akachumpia ndani ya bwawa la kuogelea upande wenye kina kirefu. Akapiga mbizi mpaka chini kabisa na akabakia huko. Edna kwa haraka akapiga mbizi kwenda kumuokoa Omari. Akafanikiwa kumuopoa kutoka katika kina cha bwawa.

Muuguzi mkuu aliposikia kitendo cha kishujaa cha Edna, maramoja akaagiza Edna aruhusiwe kutoka hospitalini kwa kuwa alimuona kuwa sasa amepona akili. Alipokwenda kumpasha habari akamwambia, "Edna, nina habari njema na mbaya kwako. Habari njema ni kwamba utaruhusiwa kurudi nyumbani kwa kuwa uliweza kuamua kwa usahihi katika janga kwa kuchumpa kwenye bwawa la kuogelea na kuokoa maisha ya mgonjwa mwingine. Nimejiridhisha kuwa kitendo chako kinaonyesha kuwa una akili njema sasa.



Habari mbaya ni kuwa Omari, yule mgonjwa uliyemuokoa, amejinyonga bafuni na taulo baada ya kuokolewa na wewe. Pole sana lakini amekufa." Edna akajibu, "Hakujinyonga, mimi nilimning’iniza pale akauke. Lini nitaruhusiwe kwenda nyumbani?"

Labels:

Monday, July 19, 2010

NIMEWAHI KUWA PWEZA

Awali ya yote nikusalimieni wote ambao mlikuja hapa lakini mkanikosa. Sababu za kutopatikana zilikuwa mbili. Mosi nilikuwa safarini ambako kulinibana hata kushindwa kupata internet. Hata nilipopata wasaa wa kuchungulia internet, sababu ya pili, mtandao haukuwepo.

Wakati wa mimi kutokuwepo hewani kombe la dunia liliendelea na kumalizika. Katika matukio yaliyonisikitisha kuhusu kombe la dunia la mwaka huu ni kutolewa 'timu yangu ya Brazil' katika hatua ya pili tu. Huwa nawapenda sana Brazil.



Flagi la Brazil

Kabla ya Kombe la Dunia kuanza nilitoa angalizo na kukata tamaa kwangu kuhusu kufanya vema Brazil. Baada ya kusikia Brazil wanakuja kucheza na Taifa Stars niliogopa na kuandika sehemu fulani maneno haya chini.Kamba unabisha soma hapa, nenda maoni ya 11

kwa nia njema tu nawaomba brazil wasije kucheza na taifa stars. stars sio kipimo cha brazil. labda ni kipimio cha kupunguza ukali wa brazil.

pili stars imekuwa ikizipa nuksi timu zinazocheza nazo kwa maandalizi ya mashindano makubwa. walianza new zealand. walipoenda afrika kusini kwenye kombe la shirikisho wakawa urojo na kutolewa mapema.

wakafuata ivory coast. walipenda angola kwenye AFCON wakawa asusa, wakatolewa mapemaa.

sasa brazil ndio wanataka kuja kupata upako wa kufanya vibaya.

kwa mashindano ya world cup mwaka huu hali ya hewa ya dar es salaam haifai kwa training. Dar ni joto, Durban ni baridi. labda brazil waende njombe.


Baada ya Brazili kutolewa nikasikitika lakini nikawa nimetabiri kama pweza paulo alivyokuwa akitabiri vyema.

Labels: ,