Friday, November 06, 2009

Kufanana, kufaana ama kufaa
Kufanana ni hali ya kitu ama mtu mmoja kuwa na sifa zinazoshabihiana na za kitu kingine ama mtu mwingine. Wakati fulani hata watu huweza kushindwa kuwatofautisha watu wafananao. Kwangu dhana ya kufanana ni ya kimaumbile tu na si ya maana zaidi ya hapo. Baadhi ya binadamu wamekuwa wakifurahia wao wenyewe ama mtu fulani kufanana na mtu mwingine aghalabu mtu mashuhuri ama tajiri. Mifano angalia hapa na hapa Mimi sichukii mtu kunanana na mtu lakini sidhani watu kufanana ni jambo la kupigiwa upatu pasi na kufikiri namna gani kufanana huko kuwe kwa manaufaa ya wote wafananao ama ya jamii kwa ujumla. Watu utawasikia huyu anafanana na rais wa nchi fulani, au mfanyabiashara fulani au mtu maarufu huyu ama yule. Mie huwa nadhani ni kupoteza muda. Mbona punda wa kijiji chenu wanafanana na wale walioko katika kijiji chetu na hawatambi wala kuwatambia watu kuwa wanafanana? Kwangu la msingi ni watu kufaana wao kwa wao ama kuifaa jamii nzima.

Labels:

Tuesday, November 03, 2009

Kasichana miaka 11 kajifungua Salama

Hivi pengine global warming inazidi kuongezeka kila mahali. Hivi sasa visichana vya miaka kumi vyaweza zaa pasi na matatizo ( angalia hata hapa). Kasichana haka ka Bulgaria Kordeza Zhelyazkova (pichani)kamejifungua salama mtoto wa kilo 2.5 na baada ya muda kakatoroka kwenda kumalizia sherehe yake ya harusi. Baba mtoto ana miaka 19. Malizia stori nzima hapa

Labels:

Tuesday, October 20, 2009

Huna Matumaini, Umekata Tamaa?

Hebu msikilize Lee Ann Womack katika I Hope You Dace, kwenye lvideo Songi hili huwa sichoki kulisikilizaga hasa ninapokataga tamaa. [wimbo umetumika pia katika filamu ya The Family That Preys]



Monday, October 19, 2009

Miaka Miwili Bila Lucky Dube

Binafsi namkumbuka sana, hasa show zake. Ninapokumbuka kifo chake (18/10/2007) cha kudungwa risasi na majahili ambao walitaka kumpora gari huwa naliwazwa na wimbo wake Crazy World. Ilisemekana wauaji wake hawakujua kuwa mtu waliyekuwa wakimuwinda alikuwa mwanamuziki mashuhuri na inadaiwa walisema: " We have killed tha man!" Kila mwaka nakumbuka mistari hii iliyopo katika Crazy World (songi kamili videoni)

People dying like flies every day
You read about it in the news
But you don't believe it
You'll only know about it
When the man in the long black coat
Knocks on your door
'Cause you're his next victim.......

Thursday, October 15, 2009

Kanumba huyo tena Jamani






Safari hii na £ovely Gamble. Trailer yake inaonyesha huyu jamaa sasa katoka kivyengine.

Starring Steven Kanumba na Mekki Macha

Director R. Okemwa

Editor B. Baraka

Producer F. Eyembe

trela iko matawi katika link hapa




Labels:

Monday, October 12, 2009

Majek Fashek then and now

I used to love the music of this Nigerian legend, Majek Fashek. I still love his music. The news has it that he is literally a pauper because of addiction to booze and some hard stuff (!).

Majek Then

I knew him because of his songs, not his addiction.


Majek Now

Today I am reminiscing with his songs especially So Long here. I really love this one. Anyone owning his CDs? I am dying for them.

Labels:

Saturday, September 12, 2009

Kufanya Mitihani na Mimba

Serikali imesharuhusu wanafunzi 'waliteleza' kufanya mitihani ya mwisho. Juzi wameanza wa darasa la saba. Nafikiri mwendo ndio huohuo kwa kidato cha nne na cha sita.



Hivi ni faida zipi na hasara zipi tuzitarajie kwa ruksa hii?

Picha kutoka kwa michuzi

Labels: