Tuesday, April 27, 2010

Ndio ishakula kwangu au?

nimejaribu kufungua mafaili yaliyomo katika flash disk yangu lakini imeshindikana. yaliyokataa kufunguka ni ya adobe na microsoft word. Sasa nikifungua ya microsoft word ndio nakutana na ujumbe huu (kwa kizunfu) hapa chini. sasa ndio ishakula kwangu kwamba siwezi kuyapata tena au nifuate masharti yake. yamo mafaili muhimu sana. nisaidieni.

Sorry I am really sorry. I don't want to do it again. This is my first and may be the last if you agree to help me.

Do you want to get your files back? That is so easy just do this. I want you to write a mail to
Zlovel_4evr@yahoo.com
stating how much I loved her.

You knowà I gave her everything I had, my heart my phaseà. all what I can and had but she gave me nothing
except pain. Now she leaves me alone and I am felling now empty inside. I can't to live without her. That is why I
burnt your files. I know may be this file is vital for you as your mail is for me. Be sure I will give your files back with
out any damage. Be sure and trust me.

Take a minute from your busy time and write a nice message to her. Then you will get all your files as befor.

Thank you for your cooperation. And I hope you will give me a pardon for my miss use of knowledge. I did it
because I left with no other option.

Labels:

Monday, April 19, 2010

WEEKEND MBAYA KWANGU



Awali ilianza kwa kuwaombea njaa Manchester United. But as I was about to celebrate Paul Scholes proved that jealousness never wins with a 30-seconds-to-go header against Man City.



Nikasema haidhuru. Huitaji mwingine afungwe ndipo wewe ushinde. Nikajua tu tutawanyuka Tottenhap Hotspur. Loh! John Terry kwanza akawazawadia penati kisha kama haitoshi 'akatafuta' mikadi iliyomtoa mchezoni.



Nikajipa moyo kuwa haidhuru. Yafaa nini kushabikia ulaya wakati wanangu wenyewe wa Jangwani wangetutoa kimasomaso dhidi ya 'hayawani'. Yale yale ya John Terry, mikadi myekundu miwili tukaipata na kugeuka asusa kwa 'hayawani' wa kariakoo. Pichani kipa wetu Obren Cuckovic akiruka bila mafanikio na kuruhusu goli la kwanza. haidhuru wao wametufunga wakati hamna sikukuu. sisi mwaka jana tuliwafunga wakati wa krismasi

Labels:

Monday, April 12, 2010

SOKOINE: MIAKA 26 KABURINI

Hayati Edward Moringe Sokoine

Ninapokuwa na nafasi huwa napenda kumkumbuka Hayati Edward Moringe Sokoine kila ifikapo tarehe 12/4, tarehe ambayo royo yake iliuaga mwili. Kwangu Hayati Sokoine atasalia kuwa shujaa wa taifa hili. Kwa kweli kwangu anashika namba ya juu sana. Pengine uadilifu na uaminifu wake ndivyo vilivyowafanya watawala wa miaka ya baadaye wajiaminishe kuwa waziri mkuu bora wa nchi hii atatoka huku alikotoka Sokoine (?). Simply the truest son Tanzania must brag to have had! Wema hawana maisha.

Tarehe kama hii mwaka 2006 nilipata wasaa wa kumkumbuka Hayati Sokoine kwa staili hii hii. Waweza soma hapa hisia zangu za wakati huo, ambazo zinasalia kuwa hivyo. Hapa chini nawashrikisha michango ya chapisho hili la mwaka 2006:

charahani said...
Mwaipopo

Kwanza umenifurahisha na kauli kuwa anayekaribia kuwa mtakatifu. Sijui protokali za kiromani nasikia sasa hivi eti wapo katika mchakato wa wenye heri halafu wakishamaliza waingie katika huo utukufu. Lakini mhh hivi pamoja na zile operesheni vijiji utakatifu utakuja kweli? (Joke)

Huyu Sokoine kuna bwana mdogo mmoja alizungumza na Bob Makani ambaye aliwahi kuwa naibu Gavana, alimnukuu akisema kuwa Sokoine aliweza kufanya kazi hadi saa tisa usiku hebu angalia hilo.

Inawezekana hili limewafanya viongozi wa sasa kuamini kuwa wamasai ni jasiri hawaogopi mtu ndiyo maana wanafikia sasa mawaziri wakuu wawili kutoka Monduli.

1:56 AM

mwandani said...
Safi Mwaipopo.
Nakumbuka kifo hicho cha Marehemu Sokoine. Nikitoka shule, njiani pale Mikoroshini (siku hizi panaitwa Namanga)nyimbo za polisi na jeshi kote redioni zilikuwa zikipiga. Nakumbuka nilifadhaika, nikasikia uchungu sana.
Hivi karibuni nilitafuta sana habari za Marehemu Sokoine kwenye mtandao nikapata chache tu ambazo hazikueleza kwa kina matendo ya marehemu.
Kumuenzi hayati Sokoine, ingelikuwa vyema kupata habari ndefu na za kina - haswa habari zinazoorodhesha sera zake - kama utekelezaji wa vita dhidi ya wahujumu uchumi... au mengineyo.

3:23 AM

Hudson Eliah Kazonta said...
Mwaipopo,

umefanya kitu muhimu sana kumkumbuka shujaa wetu aliyejitolea kupigana na mafisadi wanaoishambulia nchi yetu kwa kuitafuna kwa kutumia meno yao makali.

ukweli ni kwamba kipindi hicho nilikuwa mtaalam sana wa kulia kila nilipotakiwa kwenda shule kwani ndio nilikuwa nakaribia kufikisha miaka sita tu!

Hongera sana kaka Mwaipopo.

4:31 AM

Boniphace Makene said...
Sfi sana Baragumu, nakupongeza kwa kukumbuka huyu shujaa wetu na pia kupiga hilo dongo nimewcheka sana.

8:36 AM

Michuzi said...
baragumu unatisha! kumbe u wa falsafa hivyo? mie bwana hapa sitii neno zaidi ya kukusifia na kukutonya kwamba kaka wa mama watoto wangu (semkae kilonzo anajua) ameoa hapo monduli, hivyo nasi ni familimemba. kwa kweli ule ni ukoo takatifu, usio na makuu wala majivuno, toka wakati ule yuko hai na hadi sasa. pia ni wasomi wazuri na wachapakazi sana tu. hiyo dhana ya kuwa pm bora lazima atoke huko arusha inaweza kuwa coincidence ama sokoine ali-set precedence nasi tukaizoea hivyo kama hii dhana kwamba kuna ulazima kupeana zamu (bara na visiwani) vipindi vya urais

10:26 AM

Reginald S. Miruko said...
nimekumbuka mengi. Niliwahi kutembelea kaburi lake pale Monduli Juu, takriban km 50 kutoka mjini Arusha, wakati huo ikiwa niaka 12 baada ya kifo chake, nilikuta bado anaenziwa vilivyo, kwani 'KABURI LILIKUWA BADO LINALINDWA NA POLISI WAKATI WOTE'. Sijui sasa hali ikoje.

1:34 AM

tamba said...
Mimi kaka, nakupongeza kwa blogu yako. Nimekuwa mgeni kidogo kwenye nyanja hii na bado natengeneza ya kwangu, lakini tupo wengi na inafurahisha. Nashukuru kwa comment zako kwangu. Usikose kupitia Blogu yangu na napenda maoni zaidi na zaidi

7:23 AM

Ndesanjo Macha said...
Mwaipopo,
Inaelekea kuwa watu kama Morani Moringe wanaweza kuwa wanajitokeza nchini kwetu kila baada ya miaka 200! Ukiachilia mbali kuchapa kwake kazi, ile tabia yake ya kutopenda makuu ilikuwa ya pekee hasa ukiangalia hawa wezi wetu wa siku hizi walioko madarakani. Ingawa operesheni zake hazikuwa na nguvu ya kisheria, nia yake ilikuwa ni kuondoa uchu, uhujumu, na ubadhirifu.

Tufikirie namna gani ambayo watu kama Moringe wanaweza kukumbukwa kwa faida kubwa zaidi kuliko kutumia majina yao kwenye barabara na majengo.

5:21 AM

mwalyoyo said...
Tunakushukuru sana bw Mwaipopo kwa kutukumbusha mtu muhimu sana katika historia ya Tanzania. Nilisoma gazeti fulani makini la kiswahili linalotoka mara moja kwa wiki, kulikuwa na makala moja nzuri sana iliyohusu maisha ya Shujaa Sokoine. Nitajaribu kuwasiliana na wamiliki wa makala ile ili angalau wanablogu wengine waipate kwa njia ya mtandao. Ni jambo la muhimu sana kufahamu historia ya nguli huyu wa Tanzania. Nashukuru kwa maelezo yako ya namna ya kuanzisha blogu, nimeianza na natarajia kuweka habari mbali mbali.

Labels:

Friday, April 09, 2010

Tuikaribishe Blogu ya Maendeleo ya Jamii

Huyu jamaa E. Akyoo amekuwa muumini mzuri wa blogu za wabongo. Hatimaye naye ameona ajiunge na ulimwengu wa ku-blogu ili atujuze/atushirikishe mambo ya maendeleo ya jamii na mambo mengine pia. Hebu tukamsabahi na kumkaribisha hapa.

Labels:

Tuesday, April 06, 2010

Siku ya Afya Duniani: Malaria tunaifanyaje?

Kesho tarehe 7/4 ni maadhimisho ya siku ya afya duniani. Pamoja na mambo mengine, siku hii kimsingi hutumika kuamsha ufahamu wa magonjwa na maradhi kwa binadamu, ikiwa na lengo kuu la kujikina na kutibu ili kupunguza vifo (ingawaje mwisho wa siku wote tutakufa).

Nataka nijielekeze katika ugonjwa hatari ambao umekuwepo tangu mwanadamu awepo hapa duniani. Malaria ni ugonjwa ambao umekuwa ukiangamiza watu hata kabla ya Ukimwi. Na hata sasa. Kutokana na kuwa tishio kwa maisha ya mwanadamu nadhani kuna watu nje na ndani ya Afrika wamefanya malaria ni biashara.


Mbu akieneza malaria

Juhudi kuu dhidi ya malaria imekuwa ‘Kujikinga na mbu waenezao malaria’. Mie sikatai hoja ya kujikinga na mbu lakini nadhani ni wakati sasa tuamke na tuanzishe kitu kama ‘Tumtokomeze mbu aenezae malaria’. Hivi kwa nini tuhangaike na moshi wakati tunakujua moto uliko?

Ninashawishika kudhani katika suala zima la malaria kuna mkono wa kibiashara zaidi, biashara ambayo viongozi wetu wameingizwa ama kwa kujua ama kwa kutokujua.

Kuna jamii hapa duniani wala hazijui uwepo wa ugonjwa huu, achilia mbali kusikia. Kwa mfano, Marekani ni miongoni mwa nchi zilizoteseka sana na ugonjwa huu hususan kuanzia miaka ya 1900 mpaka mwaka 1949. Soma hapa na hapa. Wamarekani wa leo hawajui kama kuna ugonjwa hapa duniani unaitwa ‘malaria’. Hata madaktari wa huko si wote wanajua uwepo na tiba ya malaria.

Marekani yao ni hadithi ya mafanikio katika vita dhidi ya malaria. Baada ya kuangamiza watu sana, hatimaye walitokomeza malaria kwa kunyunyiza dawa ya DDT kila kona na kutoacha maji yatuame hovyo (kutengeneza miundombinu ya maji mizuri).


Vyandarua vilivyotiwa dawa 'kuzuia' mbu

Hapa ndipo hatuambiani ukweli. Wakati Marekani imefanikiwa kutokomeza mbu kwa DDT sie tunaambiwa DDT haifai na tunakubali na kupiga marufuku matumuzi ya DDT. Suala la kutengeneza miundombinu linaweza kuwa gumu kwetu kutokana na uwezo wa kiuchumi lakini nilidhani ni bora tungeambiwa tunashindwa wapi kuliko kutoambizana ukweli. Kila kukicha ‘Tujikinge na mbu waenezao malaria’.

Nijuavyo mimi vyandarua huwezesha mbu kutong’ata watu kitandani tu. Hatuambiwi kuhushu mbu aliye sebuleni, jikoni, maktaba, chooni na bafuni na kadhalika. Au tunatakiwa tuwe na vyandarua ‘vilivyotiwa dawa’ hata maktaba au sebuleni tukiwa tunacheza karata saa sita usiku? Au ‘mbu aenezae malaria’ ni yule aliyeko chumbani tu?


DDT ikipulizwa marekani kuua mbu wote

Wakati baragumu linapulizwa kwa juhudi zote‘ kujikinga na mbu waenezao malaria’, tunaona mataifa ya magharibi yanavyojenga viwanda vya vyandarua kwao na kwetu, wanavyotengeneza dawa kwao (mfano dawa mseto inatengenezwa Brooklyn, New York). Tunawaona wanapotoa misaada yenye masharti kuwa ni lazima tununue dawa kwao. Ilimradi kila uchao ni kauli mbiu za kuuhangaikia moshi ilihali tunakujua moto uliko.

Ni wakati sasa tuambiane ukweli. Tumeshakufa vya kutosha!

Labels: