Thursday, March 25, 2010

WEWE UNGEFANYEJE



umewahi kwenda bar na mkeo? soma hii..

A man went to the pub with his wife. When he left for the counter, a
prostitute approached his wife & whispered......."You must DEMAND cash before sex,
I know him very well........ He doesn't pay......!!!"

Labels:

Tuesday, March 16, 2010

MADEREVA TEKSI



Wapendwa waaminifu wa kupitiasha macho bloguni kwangu karibuni. Nilipotea hewani kidogo kwa sababu mbili; mosi ni kutokuwa na mtandao na pili kusafiri. Nilikuwa dar kwa siku 5 hivi. Nikiwa mbali na mtandao nilibahatika kusoma shairi hili hapa chini kuhusu mateksi dereva. tufuatane na mshairi mwenyewe...

Madereva wa Taxi

Na John Nkurumah Makacha (Mteule) “man of vision”

Utafiti nilofanya, Tanga na Mwanza mjini,
Na mwingine kule Kenya, hasa Mombasa Likoni,
Hakika umenifanya, nigundue ni wahuni,
Madereva wa taksi , ni wahuni wa kutupwa.

Kulamba wake za watu, kwao sio mtihani,
Kwa kutoa lifti tu, huwapata kilaini,
Wenye wake kila mtu, tahadhari chukuweni!
Madereva wa taksi , ni wahuni wa kutupwa.

Madenti wa sekondari, huwekwa vimada ndani,
Zawadi ni usafiri, ili wawahi shuleni,
Na kutaka ufahari, wawajue wao nani,
Madereva wa taksi , ni wahuni wa kutupwa.

Wana vimada lukuki, ukiwapanga foleni,
Mara leo Mama Jaki, na kesho Mama Semeni,
Kwa ngono hawatosheki, hivi wamerogwa nini,
Madereva wa taksi, ni wahuni wa kutupwa.

Kila kona wamezaa, hawana nyota kijani,
Wakikatiza mitaa, nyimbo ni baba fulani,
Una haki kushangaa, ni watu aina gani?
Madereva wa taksi , ni wahuni wa kutupwa.

Ndipo mwalimu mkuu, Makacha mwenye visheni,
Biblia nanukuu, madereva kasomeni,
Malipo ya dhambi kuu, ni kuzikwa kaburini,
Madereva wa taksi , ni wahuni wa kutupwa.


chanzo: mtanzania machi 15, 2010

Labels:

Wednesday, March 03, 2010

MAJIBU YA SAFARI YA MWANAHABARI MBEYA



Kamnara ketu

Nimebahatika kutumiwa e-mail ambayo mwandishi wake ameiita ripoti ya safari yake ya kikazi mkoani Mbeya. Ameituma kwa watu wengi ili kueneza uchafu aliouona mkoani humu. Sina uhakika nani alimpa kazi ya kuandika ripoti yake hii maana nijuavyo riporti ina kitu kinaitwa terms of reference yaani waliokutuma na jinsi walivyokutuma kufanya uchunguzi/utafiti. Lakini haidhuru pia inaweza kuwa ripoti binafsi ya muhusika anayejiita mwanahabari, ingawaje ripoti yenyewe inaonyesha alichokiandika sicho alichotumwa kufanya huko mbeya. Waweza isoma hapa
Awali napenda kumpongeza mwanahabari kwa kuonyesha yale ambayo kwa mtazamo wake hayaonwi ama hayajaonwa na watu wasiowahi kufika Mbeya ila nitachukua fursa kidogo kurekebisha yale ambayo yamewasilishwa ndivyo sivyo. Napenda ijulikane mie ni mkaazi wa mbeya kwa karibu miaka 20 mfululizo isipokuwa nikiwa shule ama vyuoni, ambako nako nilitambulika kuwa natoka Mbeya. Hivyo itambulike nina maslahi na uenyeji/ukaazi wangu hapa Mbeya.

Juhudi hii ni kwa ajili ya kuweka sawa kumbukumbu na taarifa kamili. Pili nadhani itamuongezea ufahamu bwana mwanahabari. Tatu juhudi hii itafanya upotoshajia wa makusudi wa mwanahabari pengine kutokana na wembamba wa uwezo wake wa kufikiri, kupembua na kuchanganua mambo, ujulikane.

Nianze na kunukuu mwanzo wa report yake hii. Nanukuu “Duniani kuna mambo mengi sana.” Nukuu hii inaonyesha jinsi gani huyu mwanahabari (lakini mwanahabari aliyetumwa kwenda kutengeneza mashine mbeya. Habari na umakenika wapi na wapi) alivyo maamuma wa kujua mambo hata yaliyo ndani ya nchi yake. Kwake Mbeya tu ni dunia nyingine kabisa! Kwake ilikuwa safari ya kustaabisha eti. Kwa mtu aliyefanikiwa kusafiri kuliko mwanahabari-makenika Mbeya haitofautiani sana kwa raha na mauzauza utakayoyakuta mikoa mingine, pengine mikoa mingine imeizidi hiyo Mbeya. Nitaonyesha kwa kifupi hapa chini.

Kimojawapo ni uwingi wa makanisa na sehemu za kuabudia hapa Mbeya. Eti kutoka kanisa moja mpaka lingine ni hatua 30! Nimekaa Mbeya karibu miaka 20 sijayaona hayo makanisa na viwanja vya kuabudia vilivyopakana hatua 30 kama mwanahabari-makenika anavyotaka kuwadanganya watu ambao hawajafika Mbeya.

Jambo la msingi lililonisukuma sana kujaribu kujibu ripoti hii ni maambukizi ya ukimwi mkoani Mbeya. Ni kweli Mbeya i miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa maambukizi ya gonjwa hili hatari lakini haiifuatii Johanesburg kwa maambukizi. Hata hapa Tanzania tu haishiki namba moja. Soma hapa uhakikishe. Labdha atuambie takwimu hizi kazipata wapi.

Ingawaje ripoti hii ina nia ya kutukumbusha kujiepudha na kujilinda na ukimwi lakini imejaa kejeli kama vile Mbeya na Ukimwi ni sawa na samaki na maji. Kwa mfano anasema “wenyeji wa hapa wengi hawaamini kama kuna ukimwi. Wanaamini mtu akifariki basi amefariki kutokana na mungu (sic) kumwita amechoka maisha ya dunia , wengine ndio hizo imani zao akifa mwenzao amelogwa na mambo kama hayo .” Hivi tujiulize ni kweli asilimia kubwa ya watu wa Mbeya hawajui lolote kuhusu ukimwi isipokuwa wachache na pengine wageni wanaokuja kutengeneza mashine? Kumbuka hapa alipofikia kabla hajaenda Tukuyu (alikokuita ‘mkoa’ paragrafu ya 32) na Kyela ni mjini ambako ufahamu wa uwepo wa ukimwi ni mkubwa. Au amesahau Mbeya kuna watu wanaotoka mikoa yote ya Tanzania na si kweli kuwa wote wana imani za kizamaani za washamba wa Mbeya? Kuna wachagga, wahaya, wamasai, wasukuma, wakwere n.k. Na kabila lake ‘walistaarabika’ nao wapo wanaishi hapa, na wengine hawana mpango wa kurudi huko kwa ‘wastaarabu’.

Mwanahabari-makenika anaanika kuwa hapa Mbeya “ukikutana na wasichana 5 basi 3 wanamarafiki wa kiume ambao sio wanafunzi wenzao yaani watu wa nje tu , wamachinga na madereva au watu wa shuguli zingine , hii inaadhiri sana hawa vijana utendaji wao madarasani” (para 24). Nadhani anaongelea wanafunzi lakini hajatuambia takwimu hizi amezitoa wapi ama lini yeye binafsi alifanya utafiti huu. Na pia sidhani mmomonyoko huu wa maadaili miongoni mwa wanafunzi uko Mbeya tu. Pengine kwao hamna huu upuuzi, upuuzi ambao katu siupigii upatu kokote kuwako.

Nina mashaka na tabia binafsi za mwanahabari-makenika hususani katika masuala ya ngono. Nadhani ni muumini mkuu wa kuendekeza ngono. Pengine kafikia ushemasi kabisa. Inakuwaje mtu ambaye si muendekeza ngono ukachombezana kwa simu kimahaba na wanawake asiowajua hata wakapanga siku ya kwenda Mbeya ili wakapene hilo joto (para 11) alafu anaingia mitini dakika ya mwisho. Au sitaki nataka? Pia inakuwaje mtu asiye mzinzi akaongea na msichana asiyemjua kwa masaa mawili na wakatongozana (para 38) kisha unajifanya kuingia mitini. Nashawishika kuwa mwanahabari-makenika alikuwa akina sitaki-nataka. Nilidhani mtu asiye mzinzi, kama mwanahabari-makenika anavyotuaminisha, asingejihusisha na mazungumzo yanayoshadidia ngono. Nadhani angekuwa mkali mara moja! Tena katika hili anadiliki kuwadhalilisha wasichana wa Mbeya (pasi na kuwa na uhakina ni wenyeji wa kuzaliwa hapa) kuwa ni heri atongoze ng’ombe au mbuzi kuliko wao! (para 40 & 41).

Katika mambo yote aliyoyaona Mbeya, mazuri na mabaya, aliona la ngono ndio kuu. Afrika Kusini pamoja na kuongoza kwa maambukizi ya ukimwi bado ilionekana inafaa kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia. Safari yote ya Mbeya mwanahabari-makenika ameshindwa kuona mambo chanya kama utekelezaji wa vitendo wa sera ya kilimo kwanza, hakupishana na malori yanayokimbilia Dar es Salaam yakiwa yamesheni vyakula na matunda anuai. Hakushanga hali ya hewa safi tofauti na hali ya Dar es Salaam iliyojaa sumu. Hakuona milima na mabonde yanayohitaji wawekezaji wa aina-aina. Hakuona ukarimu wa watu, wenyeji na wageni. Hakufurahia maji yasiyokatika. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Hitimisho.

Nina wasiwasi na ufahamu na uwezo wa kufikiri wa mwanahabari-makenika. Sidhani kuwa hajaenda shule kwani kusoma na kuelimika sio lazima vikatangamana. Nadhani ni wakati sote tuliolazimishwa kuisoma (ndio katutumia kwa lazima)ripoti hii tukaiangalia kwa jicho la pili. Hata majibu yangu haya pia yanahitaji upembuzi makini. Sio lazima yakawa ya kweli kwani nimeandika kwa kuzingatia maslahi ya kimkoa zaidi. Lakini nachelea mwanahabari alikuwa na nia ya kuupa mkoa wa taswira potofu zaidi ya ile iliyopo. Ni kweli mawazo yake ni baadhi ya changamoto sio tu katika Mbeya bali pia nchi nzima. Wapi hakuna mauzauza kama haya. Huko Dar es Salaam ambako mwanahabari- makenika anatoka/anaishi ndio usiseme!

Labels:

Tuesday, March 02, 2010

BARUA KWA WAZIRI WA ELIMU



[Nimeitoa taarifa hii Wanabidii Forum. Imenisikitisha. Nimeona niitundike hapa pengine/labda/may be/perhaps/ inawezekana hapa ikaonwa na mtoto mhusika akaonewa huruma.kama ni kweli basi si vema. Picha haiusiani na taarifa hii]

Mheshimiwa Waziri Suala hili imebidi likufikie kutokana na watendaji kushindwa kulishughulikia Suala la Neema Mgongo. Neema Mgongo amemaliza darasa la saba Shule ya Msingi Segerea mwaka 2008. Neema hakufaulu, Neema ana Mzazi mmoja tu yaani mama yake. Mama yake alitamani wanae asome shule ya Sekondari. Siku moja wakiwa Kanisani walitangaziwa kuwa kama kuna mtu mwenye mtoto aliyemaliza Darasa la saba Ampeleke kwenye shule inayofadhili wanafunzi na kwamba mwanafunzi atasoma kwa Tshs 100,000 kwa mwaka. Shule hiyo inaitwa KWETU HIGH SCHOOL liyoko Kunduchi Nje kidogo ya jiji la DSM.

Mama Neema alitakiwa kupeleka Barua ya serikali ya Mtaa, Shule alikosomea. Neema alipokelewa Shuleni hapo na mama yake alilipa Tshs 100,000/ mwaka 2009. Mwaka 2010 Shule hiyo imepandisha ada kutoka Tshs 100,000 hadi Tshs 200,000, Mama Neema akashindwa kulipa kiasi hicho maana hana kipato cha uhakika. Mama Neema aliomba msada serikali za Mitaa lakini hakupata msada hasa kupitia NGOs zinazosaidia Wanafunzi wazazi wao wasio na uwezo.

Katika kutafuta msada akapata habari kuwa Neema Mgongo alifaulu awamu ya pili lakini taarifa hazikumfikia kwakuwa alikuwa akiishi mbali na shule aliyosomea. Mama Neema alifika hadi Segerea Shule ya Msingi kupata Ukweli wa habari hizo. Mwalimu mkuu alimwambia ni kweli alipass kwenda Shule ya Uhuru Mchanganyiko. Mama Neema alikwenda Shule ya Uhuru Mchanganyiko akamwona Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo. Mwalimu huyo alimwambia amechelewa sana nafasi ipo ila nenda kwa Afisa Elimu akupe barua ili tumpokee. Mama Neema akachukua barua kuanzia kwa mjumbe hadi serikali ya Mtaa pamoja na Shule iliyokuwa imemfadhili. Akampelekea Afisa Elimu wa Ilala pale Boma. Afisa Elimu akasema amesoma Shule ya Private hatuwezi kumpokea. Mama Neema akamwomba amejeshee Barua alizompa akakataa kumpatia. Kesho yake akamfuatilia Afisa Elimu huyo karibu mwezi Februari 2010 wote.

Mama Neema aliomba Msaada wa Mjumbe wa Nyumba kumi. Hata hivyo Afisa huyo hakujali aliendelea kuzuia Barua hizo. Siku iliyofuata mama Neema alimwendea tena ndipo alipomtupia baadhi ya Barua hizo, Na kwamba barua ya serikali ya Mtaa na Picha alibaki nazo.

Mama Neema aliamua kwenda Wizarani kumwona Mkurugenzi wa Elimu. Wizarani Gorofa ya tatu alimkuta Mkurugenzi Chumba no 302B. Mkurugenzi huyo kabila Msukuma alimwambia aende kwa DO pale kamata jambo hilo litatatuliwa. Mama Neema alikwenda kwa DO, DO alimwambia aende Shule alikosomea Mtoto kamati ya Shule iandike barua alafu aipitishie kwa Afisa Elimu wa Ilala alafu iende kwake. Mama Neema kwa ajili ya mwanae alifuatilia barua Shule alikosoma. Kamati ikakutana na Barua ikaandikwa akapewa mama Neema akaipeleka kwa Afisa Elimu wa Ilala. Afisa huyo akaiangalia akamwambia mama Neema ipeleke kwa DO. Mama Neema aliipeleka kwa DO na DO akakubali akamwambia Mama Neema Mpelekee Afisa Elimu. Mama Neema alifikisha ile barua kwa Afisa Elimu. Afisa huyo akaipokea na kutoa sauti ya kufoka kuwa haiwezekani nimekuambia. Peeeeleka hio barua kwa DO wako. Akaendelea kufoka iache hapo nitamwandikia DO mimi mwenyewe.

Barua imekwamia kwa Afisa Elimu. Hivi DO na Afisa Elimu Mkubwa ninani? MTOTO HUYO YUKO NYUMBANI ANATAKA KUSOMA ANALIA KILA SIKU.

Labels: , ,