Friday, February 02, 2007

Sauti Ya Baragumu Yatimiza Mwaka Mmoja

Ni furaha ilioje leo kukumbuka kuwa mwaka mmoja uliopita blogu hii ndipo ilipozaliwa hapa. Na ilianza kimzahamzaha kama hivi. Kumbe blogu, pamoja na mambo mengine, ni teknolojia nzuri kutunza kumbukumbu. Binafsi nemecheeka sana kukumbuka enzi hizo!

Ingawahe ilianza kwa kishindo baadaye ilififia kidogo kutokana na mimi kurejea kwetu hapa. Si mnajua mambo ya mitandao huku. Hata hivyo azma yake ya kupashana habari bado mbichi. Pengine sasa nimeanza kutulia na kujipanga upya. "Epi bethidei" Baragumu.
Pichani nipo maabara ya kompyuta makao makuu ya chuo ninachofundisha Tanzania Institute of Accountancy, Dar es Salaam.