Monday, April 03, 2006

Ya Picha Nyingine Hiyooooo
Boniphace Makene amewahi kunidokeza kuwa kijijini anakoishi Mwananchi Communications lazima kuendelee kiblogu-blogu. Amekuwa akiwashawishi wanakijiji wenzake watandae hivi na si haba sasa tuna Yahya Charahani, Morris Mwavizo. Leo asubuni wakati nafungua kompyuta kuangalia huenda nina barua kutoka nyumbani nikakutana na mpigapicha wa kijiji hiki Mpoki Bukuku 'naye amekata shauri'. Kong'oli hapa 'ukamsilimishe'. Hala hala lakini kweni ni mbabe kwelikweli.

1 Comments:

At 4:59 AM, Blogger mzee wa mshitu said...

Mwaipopo

Baada kama ya kawiki hivi mbabe huyu aliyewatikisa askari magereza kule Ukonga na waamchangia hali iliyosababsha Omari Ramadhani mapuri apoteze umaarufu kwa kiasi kikubwa,kutinga bloguni, leo nimeamua kutembelea gazeti lako na kukuta hii.

Huyu bwana Mzee wa Sumo anatisha sijui kwanini hakuingia katika ulingo wa ndondi angalikuwa kama Tyson wa enzi zile, ingawa ana ka-chama ka wanyanyua vitu vizito

 

Post a Comment

<< Home