Friday, March 24, 2006

Mija Kategua

Pengine haikua na maana sana kupost picha ya wanamuziki mashuhuri hapo chini. Lakini kilichonipemba ni kupima ufahamu na kumbuumbu miongoni mwa watembeleaji wa kibaraza changu hiki. Kamtihani haka kalinikumba binafsi nilipoiona kwa mara ya kwanza.

Hatimaye nimeng'amua kuwa uwezo wa kumbukumbu wangu katu hauufikii ule wa mwanadada Mija Sayi. Msanii huyu bwana sio mchezo. Yeye kanitegulia kikamilifu.

Hao jamaa ndio hasa waliokuja kuwa maarufu duniani kote. Nakumbuka hata pale Mbeya Secondary School tukishindana kupata mashairi ya Bob Marley(pichani juu) ili mosi tuweze kuzielewa nyimbo zake lakini pili tufuatilie midundo ile. Yastaajabisha miaka inavyokwenda kasi namna hii hata sasa natamani kurejea maisha yale ya kishule-shule. Kwenye chapisho lililopita Bob anaonekana kushoto na tabasamu lake aliloendelea nalo hata baadaye. Kansa ilimtanguliza Bob kunako jicho la haki mwaka 1981.

Bunny Wailer (pichani kushoto) ndiye anayeonekana kwenye picha ya chapisho lililopita akiwa katikati. Ndiye mwenye jina lililotumika kuanzisha The Wailers. Bunny Wailer bado anadunda kule Jamaica.

Peter Tosh (pichani kulia) ndiye anayeonekana mrefu kuliko wenzie kulia katika picha ya chapisho la chini. Yeye ndiye aliyekng'utwa risasi na majambazi mwaka 1987 nyumbani kwake Jamaica. Huyu baadaye alijiengua kutoka The Wailers na kuanza kivyake. Mbali na kuwa watu 'walifahamu' kuwa alikuwa-ga anatumia-ga 'lile jani', yeye alikuja hadharani na kulitetea kuwa lihalalishwe.

Pichani chini ndipo wote watatu walipoanzisha The Wailers mwaka 1964. Zingine zipo hapa.