Sunday, March 26, 2006

Blogu ya Kiswahili ya Mkenya David Kiyeu Imekamilika
Pengine tunasahau hata kule Kenya Kiswahili chatumika. Basi kudhihirisha hili mwalimu wa Kiswahili kutoka Kenya anayefanya shughuli zake kule Rhode Island, David Kiyeu, 'amekata shauri' na kuona kuwa chelewa chelewa unaweza kukuta mwana si wako. Kama ilivyo ada ya waswahili mgeni siku ya kwanza tunamkaribisha kwa bashasha. Hebu tukamsalimie hapa.