Wednesday, September 22, 2010

BARUA ENZI ZA MWALIMU



Naona kati ya huyu jamaa na huyu jamaa atakayetangulia kutuma barua hii atakubaliwa na Koero Mkundi

Labels: ,

11 Comments:

At 6:42 AM, Blogger Simon Kitururu said...

:-)
Mie nakumbuka barua yangu ya kwanza ilinyunyuziwa na manukato halafu nikashindwa kumpa KIMWANA aliyekuwa ananitesa roho kisa moyo ulikuwa unadunda sana.

Halafu kwa bahati mbaya ikashikwa na dada yangu aliyetaka kunisaidia kufua nguo za shule halafu akaitembeza kwa ndugu zangu wote nyumbani kwa hiyo siri yangu ikawa imebumbuluka nyumbani.:-(

 
At 6:46 AM, Blogger John Mwaipopo said...

pole sana mkuu. lakini vipi sisteri hakukusaidia kupeleka ujembe kwa mhusika?

 
At 6:50 AM, Blogger Simon Kitururu said...

@ John: Zaidi ya kutaniwa sana sikupata msaada. Halafu tukahama Songea kwa hiyo ndio ikawa imetoka. Ila baadaye nilikuja kukutana na huyo kimwana ukubwani zaidi nikajikuta sikumbuki kwanini nilikuwa namuona bomba sana zamani. Kwa hiyo sikuhitaji tena kifuko chake cha dhambarau.


Halafu sijui kwanini WASICHANA wengi hubadilika haraka sana. Nishawahi kumpa shikamoo demu niliyesoma naye Primari kwa kuzania ni mtu wa makamo sana kunizidi.:-(

 
At 6:56 AM, Blogger John Mwaipopo said...

simeone ushawahi kufikiria kuandika kitabu ya hekaya ama hadidhi fupi fupi? au ushaandika? you have the stories that are required, man!!

 
At 7:22 AM, Blogger Simon Kitururu said...

Najaribu kuandika hekaya kadhaa! Ntakutumia uzicheki nikisha zipitia vizuri kwa mara nyingine.

 
At 8:08 AM, Blogger Fadhy Mtanga said...

kaka zangu nimecheka sana.
ukiacha zile za awali, barua maarufu ya kumwaga sera ili nipate tulizo la moyo kama siyo nafsi ilikuwa ni darasa la saba.

tulikuwa tushafanya mtihani wa taifa sasa tupo ktk maandalizi ya graduation.

nikajipinda nikaandika tenzi arobaini na mbili nikielezea hisia zangu kwa binti mmoja wa kichagga. alipoipata barua ile ambayo nyuma ya karatasi nilisihi asimwambie mtu, akamwita rafiki yake na kumsimulia.

stori zikaenea darasa zima hivyo kila mara nikawa nachekwa eti natongozea mashairi. hapakutosha na wala sikuwa na ujasiri wa kumwuliza yule binti kulikoni kamwaga mchele kwenye kuku.

nikaenda sekondari na kusahau habari zile za kukosa umaridadi pamoja na kujipinda koooote kule... nilitumia siku mbili kuidraft ile barua nikiamini kwa saundi zile dogo habanduki. aisee.

the fun thing...juzi hapa siku ya Idd si ndo nikakutana tit for tat na mwandikiwa mashairi yale baada ya miaka 15. kila mtu aliishia kucheka. swali lake la kwanza, "bado unaandika mashairi?"

unajua nilimjibu nini? nikamwambia, "unataka nikuandikie tena?"

ha ha ha ha ha aaaaaa nimekumbuka mbali sana maana naandika hii comment nikiwa hoi bin taaban kwa kicheko.

 
At 8:39 AM, Blogger John Mwaipopo said...

fadhy yako ni hadithi hai. kama nakuona unavyoandika hapa

 
At 10:26 PM, Blogger emuthree said...

Mhhh, kweli yakale yanaraha kuyasimulia, hasa enzi za shule! Nafikiri kama kungekuwa na namna ya kuhifadhi haya matukio kwenye kanda za video, tungenufaika sana `kinafsi'

 
At 1:34 AM, Blogger Yasinta Ngonyani said...

Simon na Fadhy umeniacha ho kwa simulizi zenu ama kweli watu tunatoka mbali. Ila kwa kweli hata mie imenikumbusha mbali sana. Na sikumbuki ni lini nimepata barua ila tuache mchezo ni raha sana kipata barua kama hizo zilizoandikwa kwa mkono. Naona muda si mrefu hakuna mtu atayeweza kuandika kwa kutumia kalamu na karatasi.. Ahsante kwa kumbukumbu hii!!

 
At 6:03 AM, Blogger Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Sisi kijijini kulikuwa na jamaa kabisa 'spesheli" kwa uandishi wa barua za aina hii. Tulikuwa tunamnunulia miwa, vitumbua na vitu vingine.

Umenikumbusha mbali. Mimi pia bado ninazo barua za aina hii katika makabrasha yangu; na mara moja moja huwa nazisoma. Maisha!

 
At 7:23 AM, Blogger malkiory said...

Mimi nilikuwa nikiandikiwa badala ya kuandika!

 

Post a Comment

<< Home