Saturday, September 18, 2010

ANDIKA MAELEZO YA PICHA HII



Picha hii nimeitoa hapa. Leo tushindane kuandika caption (maelezo ya picha) za kubuni wenyewe. Atakayeandika caption ya kuvutia zaidi atakuwa mshindi wetu. Namna ya kumpata mshindi nitawaambia baadae.

Labels:

3 Comments:

At 9:59 AM, Blogger malkiory said...

Mwalimu John, zawadi yangu nitumie viungo vya pilau vya Tz na siyo vya kutoka kwa watani wa jadi, nataka viungo asilia vilivyotengeneza na marashi ya Pemba. Hawa jamaa ni Marais watarajiwa, mmoja wao ni mwenye furaha na uhakika wa kushinda, na mwenzake hana raha kwa kuwa na wasiwasi wa kushindwa.

 
At 9:29 PM, Blogger o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Hiyo picha ilipigwa wakati wa shughuli ya CCBRT na hapo anaonekana mkuu wa kaya kama akimwambia:

'Nilidhani kuwa umakini wako ni bungeni tu kumbe hata huku kwenye asasi za kiraia nawe ni nguli!!!'

 
At 6:51 AM, Blogger kizito said...

Wanaongea hivi"Kikwete: Unafikiri wote uliowataja ni mafisadi? Slaa: sasa kumbe kuna niliyemuonea? Kikwete: Ndio wangine ni wala Rushwa wakubwa Sio mafisadi. Slaa: anacheka."

 

Post a Comment

<< Home