Saturday, September 12, 2009

Kufanya Mitihani na Mimba

Serikali imesharuhusu wanafunzi 'waliteleza' kufanya mitihani ya mwisho. Juzi wameanza wa darasa la saba. Nafikiri mwendo ndio huohuo kwa kidato cha nne na cha sita.



Hivi ni faida zipi na hasara zipi tuzitarajie kwa ruksa hii?

Picha kutoka kwa michuzi

Labels:

6 Comments:

At 8:48 AM, Blogger Simon Kitururu said...

Naamini faida mojawapo ni kuwasaidia waliobebeshwa kijaza dunia kuweza kujiendeleza kirahisi kielimu baada ya kumaliza kusaidia kuujaza ulimwengu

 
At 10:00 AM, Blogger Bennet said...

Tunatakiwa kuachana na adhabu bali wale waliokosea wanahitaji kurekebishwa, hii ndio njia moja wapo lakini inabidi tuwe makini kidogo

 
At 12:33 PM, Blogger Yasinta Ngonyani said...

Haraka haraka haina baraka . Tutafika tu huko. Ila mi sijaelewa kwa nini wasichana wanaobeba mimba wasiendelee na masomo yao kama kawaida au baada ya kuzaa?

 
At 7:03 AM, Blogger Christian Bwaya said...

Kama wa kiume wanaachwa kufanya mtihani, kwa nini hawa wa kike wasifanye? Tabia zao zinafanana, isipokuwa huyu wa kike anabeba kidhibiti!

 
At 8:45 AM, Blogger chib said...

Bwaya! Weye una akili sana

 
At 9:23 PM, Blogger Mzee wa Changamoto said...

Faida ni kuwa hata ambao walikosea wanaweza kupata nafasi ya pili kujirejea. Na kwa kuwa wanakuwa na "chungu" ya maisha, wanaweza kuwa makini zaidi.
Hasara ni kuwa wasio na akili wataona kuwa hawana la kuhofia (japo si ukweli) kwa kuwa tu hata wakipata mimba watasoma.
Kuwatisha na kuwaadhibu kabla ya kuwaelimisha ni kutwanga maji
TUWAELIMISHE WAJITAMBUE NA KUTAMBUA HASARA NA ATHARI ZA MATENDO YAO
Blessings

 

Post a Comment

<< Home