Friday, October 17, 2008

Mwaka Mmoja bila Lucky Dube
Kesho tarehe 18/10/08 tasnia ya muziki wa reggae itaadhimisha mwaka mmoja toka siku ile chungu ya kuuwawa kwa risasi wa nguli wa muziki huo wa kule africa kusini, hayati Lucky Philip Dube.
Akifanyaga vitu vyake watu walikuwaga nyomi. Sehemu nyingi ama ilikuwa wauane kwa kukanyagana ama ndugu wapoteane

Katoy kalikomponza hata majahili wakamtoa roho wakitaka utajiri wa fasta-fasta. Hapo ndio eneo la tukio alipojaribu kushindana nao na kisha kuugongo huo mti akiwa amekufa tayari.

Maziko yake. Tandiko majani, blaketi udongo.

Pengine alitabiri kifo chake katika wimbo Crazy World kutokana na uhalifu wa namna hiyo kukithiri Afrika ya Kusini. Ubeti mmoja unaenda hivi:

So far so good we still living today

But we don't know what tomorrow brings

In this crazy world

People dying like flies every day

You read about it in the news

But you don't believe it

You'll only know about it

When the man in the long black coat

Knocks on your door

'Cause you're his next victim

As you are living in this... (crazy world)

Kwaheri Lucky Dube

Labels:

2 Comments:

At 10:00 AM, Blogger Fita Lutonja said...

Nimefuhia zaidi mimi natamani kuikomboa Tz

 
At 10:41 AM, Blogger Fadhy Mtanga said...

Lucky Dube alikuwa ni zaidi ya mwanamuziki, zaidi ya mwanafalsafa.
Ukiutafakari ujumbe ndani ya muziki wake, hakika nafsi yako itakiri kuwa dunia, si tu imempoteza mpiganaji mahiri, bali mwanafalsafa aliyebobea. Mwanafalsafa ambaye hakuchoka kuonesha njia.

 

Post a Comment

<< Home